Tunaendelea pale pale tulipoishia sehemu ya tatu baada ya yule binti aliyepewa jukumu la kumfuatilia kelvin kuwapoteza kipindi anaongea na Goodluck ambaye ndiye aliyempa kazi ya kumfuatilia kelvin. Basi yule mzee alimuonyesha nyumba na alikuwa kamuandalia kila kitu ndani kuanzia Godoro na vitu vingine vidogo vidogo kama mahitaji hakika kelvin alifurahi sana na kuona kuanza kwake upya kumekuwa ni rahisi sana .Lakini shukrani nyingi ziende kwa mzee Ismaili kwa moyo wake wa upendo kwa kijana kelvin .
TURUDI TENA KWA KINA ALICE
(BAHARINI)
Bahari huko Alice alimwomba dada yake anaenda kwa binadamu kukutana na kelvin dada yake alimkataza sana lakini wapi Alice alimuomba sana dada yake naye alimpa ruhusa kuwa leo hata enda ila kesho ndo atamruhusu hivyo ajikaze tu .
Alichukia sana Alice lakini hiyo haikumfanya dada yake amruhusu aende kwa wanadamu basi siku hiyo ilipita kesho yake majira ya asubuhi kelvin kaandaa mtumbwi wake tayari kwenda kuvua samaki ili angalau afanye biashara aweze kuboresha nyumba yake na kununua vitu maana anaamini kwa jinsi alivyo na wateja hakuna linaloshindikana.
Basi lakini akiwa bize na mambo yake
mara ghafla nyuma yake alitokea Alice chapu …..
si unajua si kiumbe cha kawaida muda huo kelvin ana set set mambo yake . Ghafla akasikia sauti kwa nyuma yake “umefanya uamuzi sahihi sana ” huku Alice akipiga makofi …
Kelvin aligeuka na kuachia nyavu chini maana alikuwa amemshtuka na kusema “ooooooh kumbe ni Alice ,maana umenishtua sana “
“hahahaha kweli kelvin am sorry basi maana nilitaka nikufanyie suprise tu Sikujua kama nitakufanya ushtuke “
“hapana hata usijali mmmmmh siku ile
ulipotea potea tu nageuka mara vuuuh haupo??? ” aliuliza kelvin
” anhaaa ile siku niliona kama unachelewa chelewa nikaamua nikukimbie ila nilifika nyumbani salama tena mapema hivi we hukunyeshewa ???” alijibu na kuuliza Alice
kelvin alimjibu “siku nyeshewa sana ilikuwa kawaida tu yaani niliwahi mapema nikajificha kwa jirani yangu mmoja hivi mpaka mvua inaisha mambo mengine yakaendelea ita tabia mbaya
ulinikimbia …. hii inaonyesha jinsi gani
unaogopa mvua Alice …..”
Basi walizungumza kwa muda mrefu sana lakini ngoja nikuibie siri usiojua kuhusu NGUVA
NGUVA anapokuwa nchi kavu hatakiwi kabisa kunyeshewa na mvua wala kuguswa na maji yoyote yale maana kama ikitokea hali hiyo hapo hapo anabadilika na kuwa nguva .na kwa kipindi hicho ilikuwa ni vita kubwa kati ya jamii ya Nguva na binadamu . Ndo maana siku ile Alice alikimbia kama upepo kurudi katika jamii yao kabla hajanyeshewa na mvua maana hali hiyo itaweza kuhatarisha maisha yake
……
Basi tuendelee baada ya mazungumzo
marefu sana kelvin alimwambia Alice ni muda sasa wa kwenda kutafuta samaki Basi kabla hajaenda Alice alisogea na kugusa nyavu za kelvin huwezi amini mwanga wa bluu ulitokea kuanzia mikononi mwa Alice kutapakaa kwenye nyavu nzima lakini huwezi amini kelvin hakuweza kuona chochote kile maana tukio hilo ni nje ya upeo wa macho ya binadamu,mwishowe alimwambia unaweza kwenda kelvin …….
Kelvin aliingia majini na baada ya masaa mawili alirudi akiwa amechoka sana na watu wengi walikuwa wakimsubiri ata Alice naye alikuwa yupo hapo hapo ana
msubiri kelvin alionekana kuwa na furaha
sana , Samaki walikuwa ni wengi kuliko kawaida yaani kelvin alijisemea moyoni mwake “mbona siamini kweli mungu ni mkubwa leo nitauza sana samaki na nitakifanyia ukarabati kile chumba alifika mpaka ufukweni ambapo wapo watu na kuwambia wasogee ili wapate samaki …
watu walisogea cha ajabu alimuona Alice akamwambia “bado upo tu nikajua ushaondoka anyway utanisaidia kuuza
….”
waliuza kwa muda mrefu sana na baadaye walimaliza aisew walipata hela sana maana samaki waliopata walikuwa ni wakubwa hivyo bei nayo ilikuwa kubwa
Kama kawaida wavuvi wengine walizidi
kumchukia lakini yeye hakujali waliondoka na Alice wakiwa na hela nyingi sana nakuelekea kwenye nyumba aliyopanga . kelvin mpaka sasa hajuwi kuwa alice ni NGUVA na hata uwingi wa samaki chanzo ni yeye mwenyewe Alice
….. Basi walipokuwa wakitembea kelvin alimwambia nashangaa nimekuzoea ghafla tu
Alice alicheka na kusema “hakika ni kawaida tu kelvin sisi ni people sio milima “
lile tabasamu la Alice lilimfanya kelvin abaki tu akimtazama na mawazo yakienda mbali alijisemea kimoyomoyo “wewe ni
mzuri Alice jamani mungu anaumba
daaah”
Alice aliyasikia maneno hayo japo kelvin aliongea kimoyomoyo duuuuuh Alicheka na kusema “asante sana kelvin huku akicheka …
Asante ya nini Alice …….. ????? aliuliza kelvin maana hakumfanyia chochote wala kusema chochote
Alice alimjibu “kwa kila kitu tu et naenjoy tu kukutana na wewe hakika unanifanya nifurahi ” kelvin alicheka na kusema wewe pia unanifanya hivo ….
Mwisho wa siku walikuwa washafika nyumbani kwa mzee ismaili ambapi kelvin
aliamua kupelekea samaki wakubwa
watatu kama shukrani …….
Alifika na kumuita ” baba nimerudi baba njoo uchukue zawadi yako njoo haraka
zee Ismaili alitoka mbio mbio lakini alipotoka nje alimuona Alice yule mzee alishtuka je sababu ni nini usikose sehemu ya 5
0 Comments